Kerry asema Somalia inabadilika

John Kerry amekutana na rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud leo pamoja na waziri mkuu na viongozi wa majimbo katika uwanja wa ndege wa Mogadishu.
Katika ajenda za mkutano huo mapambano dhidi ya kundi la al-Shabaab lilikuwa suala kuu, pamoja na majeshi ya Afrika na ndege za Marekani zisizokuwa na rubani.
Majeshi hayo na ndege hizo zimedhoofisha uongozi wa kundi la al-Shabaab katika miaka ya hivi karibuni na kuliacha kundi hilo bila ya maeneo makubwa ambayo lilikuwa linadhibiti, ama fedha zinazohitajika kujijenga upya.
No comments:
Post a Comment